Harurururururuuuuuuuuuuu. Nikikumbuka hivi vigeregere huwa nacheka peke yangu yaani siamini kuwa sasa imeshafika miaka MINNE tangu watu wapige Vigeregere hivi kwangu siku nilipokuwa naoa. Naam Leo tarehe 29/07/2010 nimetimiza miaka MINNE tangu nilipopiga goti na kukabidhiwa Bi. Fauzia Edward Chami ambaye kwa sasa anaitwa 'MAMA RAHMARITAH'
Mke wangu Mpenzi Fauzia Chami (MAMA RAHMARITAH)
Ninaamini sio mapenzi yangu wala ya Bi. Fau yaliyosababisha tufike hapa tulipo ama yaliyosababisha tudumu kiasi hiki ambacho si kikubwa sana lakini pia si kidogo kwa maana tumeshuhudia ndoa nyingi zilizofungwa baada yetu zikavunjika ndani ya mwaka ama miezi kadhaa tu, haya yote ni mapenzi ya Muumba afanyaye yote haya ka makusudi yake. Mimi na mke wangu tunasema ALHAMDULILLAH na tunamuomba Mungu atuzidishie miaka ya kuishi pamoja, macho ya husda yasituangukie. Amin.
Mwozeshaji alinikabidhi binti huyu kwa kusema "Nimekuozesha" nami nikajibu "Nimemuoa" wamama wakaitikia kwa vigeregere "Rurururururururuuuuuu"

