Tuesday, September 22, 2009

Tumejifunza nini?


Katika kila jambo ambalo mwana wa Adam analifanya na kwa uwezo wa Rabbana likafanikliwa, basi hakuna buni kwa Mwana wa Adam huyo kumshukuru kwalo.
Naam, Takriban mwezi mzima waumini wa dini ya Kiislam walikuwa katika mfungo mtukufu wa Ramadhani. Mfungo ambao ni mojawapo ya nguzo kuu za Uislam. Kwa mafundisho ya vitabu vitukufu vya Iman ya Kiislam Ramadhan ni Mwezi ambao Mja anatakiwa ajikurubishe kwa Mola wake ili kubata Toba na Msamaha wa dhambi zake. Katika Ibada zote ambazo Watu wameamrishwa kuzifanya, hii imeonekana ni Ibada ya pekee kutoka na watu wengi kuitii na kuifuata. Kitu kinachosababisha hata wasio waumini wa Dini hiyo kuhisi kuwa ]kuna ulazima wao pia kuwa watulivu na wengine kuungana nao katika SWAUM.

Hii inathibitika kwa mifano kadhaa katika jamii ikiwemo kupungua kwa idadi kubwa ya watu waliokuwa wakihudhuria sehemu za starehe na mabaa mbalimbali kama ilivyokuwa hapo awali kabla ya Mwezi huo (Ramadhani) kuingia na kuwatuliza watu.

Ama kwa hakika Dunia ilikuwa Shwari kutokana na kupungua kwa kiasi kikubwa kwa maasi.

Lakini sasa, Swali linakuja kwetu; TUMEJIFUNZA NINI kutokana na Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ambao umetuacha na hautakuja tena mpaka Mwakani ambapo mimi na wewe hatujui kama utatukuta?

Je, kuondoka kwa mwezi iwe ndiyo fursa kwetu kujiunga tena na tabia za kumuhasi Muumba?

Mi nawatakia Maisha mema na ningependa pia kuwaasa ndugu zangu pamoja na kuiasa nafsi yangu juu ya kumcha Mola ambaye uwepo wake ni wa DAIMA na endapo tutarudia matendo maovu ambayo tulikuwa tukiyafanya awali (kabla ya Ramadhani) tutakuwa ni watu ambao tulikuwa tunaiabudu Ramadhani na si Mungu ambaye ameileta Ramadhani ilim iwe Kifutio cha Dhambi zetu.

Nawatakia kila la kheri katika maisha yenu ya kila siku.


PashalOnline